Pata taarifa kuu
KENYA-HARAMBEE STARS-SOKA

Wachezaji wa Harambee Stars waahidiwa kitita cha pesa

Shirikisho la Soka nchini Kenya (FKF), limetangaza mfumo utakaotumiwa kuwalipa marupurupu wachezaji wa timu ya taifa Harambee Stars watakaoshiriki katika fainali ya bara Afrika nchini Misri, kati ya mwezi Juni na Julai mwaka huu.

Sebastian Migne (Kushoto) kocha mpya wa Harambee Stars, akitambulishwa rasmi na rais wa Shirikisho la soka nchini Kenya FKF Nick Mwendwa (Katikati) jijini Nairobi Mei 03 2018
Sebastian Migne (Kushoto) kocha mpya wa Harambee Stars, akitambulishwa rasmi na rais wa Shirikisho la soka nchini Kenya FKF Nick Mwendwa (Katikati) jijini Nairobi Mei 03 2018 FKF
Matangazo ya kibiashara

Rais wa FKF Nick Mwendwa, amesema kuwa wachezaji wote 23 na kocha Sebastian Migne watalipwa Shilingi za Kenya 750,000 sawa na Dola 7,500 kipindi chota watakachokuwa nchini Misri.

Mbali na malipo hayo, kila mchezaji atalipwa Dola 2,500 sawa na Shilingi 250,000 kwa kila mechi watakayoshinda.

Serikali ya Kenya imetenga bajeti ya Shilingi za nchi hiyo zaidi ya Milioni 200 kuisaidia Harambee Stars katika mashindano hayo.

Droo ya fainali hii itafanyika siku ya Ijumaa jijini Cairo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.