Wachezaji wa Harambee Stars waahidiwa kitita cha pesa
Shirikisho la Soka nchini Kenya (FKF), limetangaza mfumo utakaotumiwa kuwalipa marupurupu wachezaji wa timu ya taifa Harambee Stars watakaoshiriki katika fainali ya bara Afrika nchini Misri, kati ya mwezi Juni na Julai mwaka huu.
Imechapishwa:
Rais wa FKF Nick Mwendwa, amesema kuwa wachezaji wote 23 na kocha Sebastian Migne watalipwa Shilingi za Kenya 750,000 sawa na Dola 7,500 kipindi chota watakachokuwa nchini Misri.
Mbali na malipo hayo, kila mchezaji atalipwa Dola 2,500 sawa na Shilingi 250,000 kwa kila mechi watakayoshinda.
Serikali ya Kenya imetenga bajeti ya Shilingi za nchi hiyo zaidi ya Milioni 200 kuisaidia Harambee Stars katika mashindano hayo.
Droo ya fainali hii itafanyika siku ya Ijumaa jijini Cairo.