KAGAME CUP-SIMBA-GOR MAHIA-AZAM-CECAFA
Nusu fainali ya Kagame Cup kuchezwa kesho
Michuano ya Kombe la Kagame inaendelea kesho kwa mechi za nusu fainali ambapo Simba itachuana na JKU ya Zanzibar.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Mchezo mwingine utakuwa baina ya Gor Mahia na Azam.
Simba iliishinda AS Sports ya Djibout katika robofainali na JKU iliishinda Singida United kwa mikwju ya penati 4-3 katika robo fainali baada ya kutoka suluhu kwa dakika 120.
Mabingwa wa Kenya Gor Mahia waliiondoa Vipers ya Uganda kwa mabao 2-1 nayo Azam jana iliilaza Rayon Sports kwa mabao 4-2.
Mashindano hayo yanayofanyika kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2015 yatafikia tamati Julai 13 kwa mchezo wa fainali na ule wa kusaka mshindi wa tatu.