Pata taarifa kuu
TFF-UGANDA-TANZANIA

Azam yamsajili beki wa Timu ya Taifa ya Uganda

Klabu ya Azam imeendelea kuimarisha kikosi chake baada ya kumsajili beki wa kimataifa wa Uganda, Nicholaus Wadada.

Beki wa kimataifa wa Uganda, Nicholaus Wadada (kushoto)akisaini mkataba wa kuitumikia Azam
Beki wa kimataifa wa Uganda, Nicholaus Wadada (kushoto)akisaini mkataba wa kuitumikia Azam Mwanaspoti
Matangazo ya kibiashara

Wadada mlinzi wa pembeni amesajiliwa kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea klabu ya Vipers ya Uganda.

Kabla ya kusajiliwa na Azam, Wadada pia alikuwa akitajwa kuwaniwa na Simba na Yanga.

Anakuwa mchezaji wa nne kusajiliwa na Kocha mpya wa Azam, Hans Pluijm. Wengine waliosajiliwa ni Tafadzwa Kutinyu, Donald Ngoma na Ditramu Nchimbi.

Aidha klabu hiyo imefanikiwa kumrejesha kundi mchezaji Mudathir Yahya ambaye msimu uliopita aliitumikia Singida United.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.