Michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kuchezwa Jumatano hii
Michezo kadhaa ya hatua ya makundi ya taji la Shirikisho Afrika inachezwa leo. Katika Kundi D Yanga ya Tanzania inaipokea Rayon Sports katika Uwanja wa Taifa mchuano ambao ni muhimu sana kwa Yanga
Imechapishwa:
ikiwa inataka kusonga mbele katika hatua ya robo fainali.
Mchezo mwingine wa kundi hilo utakuwa baina ya Gor Mahia ya Kenya ambayo inaipokea USM Alger ya Algeria.
Mechi nyingine za taji la Shirikisho ni kama ifuatavyo:
Asec Mimosas itakuwa ugenini nchini Kongo kuchuana na AS Vita
Adouana Stars itachuana na Raja Casablanca
UD Songo na RS Berkane
Al Hilal na Al Masry
CARA Brazaville na Enyimba
Djoliba ya Mali itakumbana na Williumsville ya Ivory Coast