EVERTON-SAM ALLARDYCE-MARCO SILVA
Klabu ya Everton yamfuta kazi Kocha wake Sam Allardyce
Klabu ya Everton imetangaza kumfuta kazi Meneja wake Sam Allardyce ikiwa imepita miezi sita tangu alipochukua jukumu la kuinoa timu hiyo.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Ripoti kutoka nchini Uingereza zinasema uamuzi huo umefikiwa ikiwa ni sehemu ya mikakati ya mmiliki wa timu hiyo .
Big Sam ameiongoza timu hiyo katika mechi 26 akishinda mechi 10 kutoka sare michezo saba na kufungwa mechi tisa, na ameiongoza timu hiyo kumaliza katika nafasi ya nane kutoka 13 alipoichukua katika Ligi Kuu ya England.
Inaelezwa Kocha wa zamani wa Hull City na Watford Marco Silva atachukuaa jukumu la kuinoa timu hiyo.