BURUNDI-AFRIKA-JUDO-MICHEZO-
Mashindano ya bara Afrika kuwania taji la mchezo wa Judo Kuanza Burundi
Mashindano ya bara Afrika kuwania taji la mchezo wa Judo yataanza siku ya Alhamisi jijini Bujumbura nchini Burundi. Mashindano hayo yatazishirikisha nchi 13 kutoka Afrika.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Wachezaji 66 kutoka mataifa 12 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano hayo makubwa kwa vijana barani Afrika.
Kati ya wachezaji hao, wachezaji 35 ambao wanafahamika kama Judoka, ni wanaume huku wanawake wakiwa ni 31.
Mataifa yanayoshiriki ni pamoja na Algeria, Djibouti, Misri, Gambia, Cote d'Ivoire, Madagascar, Morocco, Senegal, Afrika Kusini, Tunisia, Zambia na Zimbabwe.