Hispania, Brazil na Ufaransa zapata ushindi mechi za kimataifa za kirafiki
Mataifa ya Ufaransa, Hispania na Brazil yameibuka na ushindi katika mechi za kimataifa za kirafiki zilizochezwa katika miji mbalimbali duniani.
Imechapishwa:
Mechi hizo zinachezwa kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Kandanda Duniani (Fifa), zilizochezwa jana.
Hispania ambao walikuwa mabingwa wa kombe la dunia mwaka 2010 wailipata ushindi mnono wa mabao 6-1 dhidi ya Argentina huku mshambuliaji wa Real Madridm Isco akifunga mabao matatu, Ufaransa iliwachapa wenyeji wa Kombe la Dunia mwaka huu, Urusi kwa mabao 3-1.
Timu nyingine zilizopata ushindi ni Brazil ambayo iliwachapa mabingwa wa Kombe la Dunia, Ujerumani kwa bao 1-0 lililofungwa na Gabriel Jesus. Croatia iliichapa Mexico kwa bao 1-0 na Peru iliichapa Iceland kwa mabao 3-1 nayo Ubelgiji iliishinda Saudi Arabia kwa mabao 4-0.
Wawakilishi wa bara la Afrika katika Kombe la Duniam Misri walishindwa kutamba mbele ya Ugiriki kwa kufungwa kwa bao 1-0 wakati wawakilishi wengine wa Afrika, Tunisia waliishinda Costa Rica kwa bao 1-0.
Matokeo ya mechi nyingine za kirafiki zilizochezwa jana
Italia ilifungana bao 1-1 na England
Bosnia&Herzegovina ilitoka suluhu na Senegal
Denmark pia ilitoka sare ya bila kufungana na Chile
Ivory Coast iliichapa Moldova kwa mabao 2-1
Romania iliifunga Sweden kwa bao 1-0
Iran pia iliifunga Algeria mabao 2-1
Georgia iliifunga Lithuani mabao 4-0