Samuel Muchai atajwa mchezaji bora nchini Kenya
Mwanariadha wa Kenya Samuel Muchai ametajwa kuwa mwanamichezo bora kwa mwaka 2017, baada ya kupigiwa kura na wanahabari wa michezi nchini humo.
Imechapishwa:
Muchai ambaye ni mwanariadha mlevu, alishinda tuzo hiyo inayofahamika kama SOYA baada ya kushinda medali mbili za dhahabu wakati wa mashindano ya Olimpiki kwa walemavu mwaka 2016 nchini Brazil.
Tuzo ya Wanariadha wa mwaka iliwaendea Hellen Obiri na Conseslus Kipruto.
Wawili hao walishinda medali ya dhahabu katika mashindano ya riadha ya dunia mwaka uliopita jijini London nchini Uingereza.
Obiri mwenye umri wa miaka 28 alishinda mbio za Mita 5,000 huku Kipruto akiibuka wa kwanza katika mbio za Mita 3,000 kuruka viunzi na maji.
Orodha kamili Washindi:
Mwanamichezo bora wa mwaka
Samuel Muchai (Mwanariadha mlemavu)
Mchezaji bora wa kiume
Conseslus Kipruto (Riadha)
Mchezaji bora wa kike
Hellen Obiri (Riadha)
Mchezaji bora chipukizi kwa upande wa kiume
Aman Gandhi (Cricket)
Mchezaji bora chipukizi kwa upande wa kike
Jackline Wambui (Riadha)
Mchezaji bora anayeishi na ulemavu (Kiume)
Samuel Muchai (Paralympics)
Mchezaji bora anayeishi na ulemavu (Kike)
Beryl Wamira (Deaflympics)
Kocha bora wa mwaka
Jimmy Kamande (Cricket)
Timu bora ya mwaka-Kiume
Timu ya taifa ya Cricket chini ya miaka 19
Timu bora ya mwaka-Wanawake
Kenya Lionesses (Raga)
Shirikisho bora la mwaka
Riadha Kenya
Wachezaji mashuhuri
Allan Thigo(Soka) and Stephen Muchoki (Bondia)