Rooney akabiliwa na kosa la kuendesha gari akiwa mlevi
Wayne Rooney, nahodha wa zamani wa kikosi ya ingereza cha Manchester United, anatatajiwa kuripoti mahakamani leo Jumatatu baada ya kushtumiwa kuendesha gari akiwa mlevi.
Imechapishwa:
Nyota huyo natarajiwa kufika mahakamani katika mji wa Stockport siku moja baada ya kurejea Old Trafford kwa mara ya kwanza tangu ajiunge na Everton.
Bw. Rooney alikamatwa wakati polisi walisimamisha gari lake katika eneo la Wilmslow, jijini Cheshire Septemba mosi.
Hata hivyo Wayne Rooney mwenye umri wa miaka 31, mzaliwa wa Liverpool, aliachiliwa kwa dhamana baada ya kushtakiwa kwa kuendesha gari akiwa mlevi.
Wayne Rooney, baba wa watoto watatu anashikilia rekodi ya kufunga mabao mengi zaidi nchini Uingereza.