Pata taarifa kuu
TOUR DE FRANCE

Chris Froome aelekea kushinda Tour de France mwaka 2017

Chris Froome anaelekea kushinda taji lake la nne la makala ya 104 ya kukimbiza Baiskeli ya Tour de France.

Chris Froome (Aliyevalia sare ya njano) akishiriki katika mashindano ya Tour de France
Chris Froome (Aliyevalia sare ya njano) akishiriki katika mashindano ya Tour de France REUTERS/Christian Hartmann
Matangazo ya kibiashara

Froome raia wa Uingereza, yupo katika nafasi nzuri licha ya Mfaransa Warren Barguil kumaliza wa kwanza katika mzunguko huo wa 18 siku ya Alhamisi baada ya kushinda umbali wa Kilomita 179.5 kati

Siku ya Ijumaa wakimbiza Baiskeli wanapambana katika eneo tambarare, kutoka Embrun kwenda Salon-de-Provence.

Jumamosi itakuwa ni zamu wa wakaazi wa mji wa Marseille kujionea wakimbiza Baiseli hao kabla ya kumalizika kwa mashindano hayo siku ya Jumapili kutoka Montgeron kwenda jijini Paris umbali wa Kilomita 103.

Hadi kumalizika kwa mashindano ya mwaka huu yaliyoanzia nchini Ubelgiji na Ujerumani, mapema mwezi huu watakuwa wamemaliza Kilomita 3,540.

Waandalizi wa mashindano haya watatumia Euro 2,280,950 kuwazawadia wakimbiza baiskeli watakaomaliza katika 160 bora.

Mshindi atapata Euro 500,000, mshindi wa pili Euro 200,000 na mshindi wa tatu atakabidhiwa Euro 100,000.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.