Pata taarifa kuu
CHAN 2016-TUNISIA-GUINEA-NIGER-NIGERIA

CHAN 2016: Tunisia na Guinea zafuzu robo fainali

Timu za Guinea na Tunisia wameshindia nafasi zao katika robo fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika, Jumanne hii Januari 26 nchini Rwanda. Guinea imeimenya Nigeria 1-0, nayo Tunisia ikaiburuza Niger mabao 5-0. Ngeria na Niger wameondolewa katika michuano hiyo.

Timu ya Tunisia katika michuano ya CHAN 2016.
Timu ya Tunisia katika michuano ya CHAN 2016. Courtesy of cafonline
Matangazo ya kibiashara

Tunisia na Guinea zote kutoka kundi C zimefuzu robo fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika, CHAN 2016. Tunisia, mshindi wa makala 2011 imejikuta imeimenya Niger mabao 5-0, na hivyo kuipelekea kufuzu katika robo fainali. Guinea, ambayo ni kwa mara ya kwanza inashiriki michuano hii ya CHAN 2016 imebahatika kuingia katika hatua hii.

Mchuano kati ya Guinea Nigeria umechezwa katika uwanja wa mpira wa Rubavu. Ibrahima Sory Sankhon aliipatishia timu yake ya Guinea bao moja peke la ushindi katika dakika ya 45. Tunisia yao unhooked dhidi Niger, shukrani kwa Saad kipekee Bguir katika kipindi cha kwanza.

Upande wa timu ya Tunisia, bao lake la kwanza limeingizwa katika dakika ya 5 ya mchezo na mshambuliaji wa klabu ya Espérance Tunis, Saad Bguir. Mchezaji huo mahiri alifunga bao la pili katika dakika ya 39, baada ya mpira kugonga mwamba: 0-2.

Beki wa Niger Musa Shehu alionyeshwa kadi ya manjano. Katika dakika ya 73, Youssouf Oumarou Alio, aliondolewa uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu, na hivyo Niger ikasalia na wachezaji kumi pekee uwanjani.

Hatma ya Niger

Bao la tatu la Tunisia limefungwa na Akaichi katika dakika ya 78, huku Amine Ben Amor akifunga bao la nne katika dakika ya 81. Hatimaye, Hichem Essifi alimalizia kwa bao la tano katika dakika ya (90 + 2).

Kwa ushindi huo, Tunisia imemaliza ikiwa ya kwanza katika Kundi C mbele ya Guinea, kufutia tofauti ya mabao. Januari 31 mjini Kigali, timu za kundi D, Zambia, Mali na Uganda zitajitupa uwanjani.

Timu za kundi C jinsi zinavyoshindana

1. Tunisia pointi 5 – imefuzu
2. Guinea pointi 5 – imefuzu
3. Nigeria pointi 4 – imeondolewa
4. Niger pointi 1 – imeondolewa

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.