Pata taarifa kuu
SOKA-CHAN

Libya yatwaa ubingwa wa michuano ya CHAN mwaka 2014

Timu ya Taifa ya Libya imetwaa ubingwa wa kombe la mataifa ya Afrika CHAN mwaka 2014 katika michuano iliyomalizika mwishoni mwa juma hili nchini Afrika Kusini.

Matangazo ya kibiashara

Libya imetwaa taji hilo kwa kuifunga Ghana mabao 4-3 kwa mikwaju ya penati baada ya dakika 120 za mtanange huo kumalizika kwa sare ya bila kufungana.

Hili ni taji la kwanza la kimataifa katika mchezo wa soka kutwaliwa na Timu ya Taifa ya Libya kupitia michuano ya CHAN ambayo huwashirikisha wachezaji wanaocheza ligi za nyumbani pekee.

Matokeo hayo yameamsha shamrashamra za wapenzi wa soka katika mji mkuu wa Libya Tripoli ambapo mashabiki wamekesha mitaani wakishangilia ushindi huo.

Katika mchezo wa awali wa kusaka nafasi ya mshindi wa tatu, Nigeria iliifunga Zimbabwe bao 1-0 na kujinyakulia medali ya shaba ya michuano hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.