Pata taarifa kuu
Serbia

Serbia hatarini kushukiwa na rungu la FIFA

Shirikisho la soka nchini Serbia SFA huenda likakumbwa na rungu la FIFA kufuatia machafuko yaliyozuka katika mchezo kati ya timu ya Taifa ya Serbia dhidi ya Wales na kupelekea kuvurugika kwa mechi hiyo ya kufuzu kwa kombe la dunia.

Matangazo ya kibiashara

FIFA imethibitisha kuwa bado ipi katika mchakato wa kupeleleza tukio hilo lililotokea Septemba 11 pale Wales walipopachikwa mabao 6-1.

Rungu la FIFA litawashukia pia watakaobainika kuhusika na tukio jingine kama hilo ambalo lilijirudia mwezi Oktoba kwenye mechi kati ya Croatia na Macedonia ambao nao wapo katika kundi hilo.

Kesi zote hizo zitasikilizwa na kamati ya nidhamu ya FIFA Novemba 20, mwaka huu wakati Shirikisho la kandanda barani Ulaya kwa upande wake limetenga Novemba 22 kama siku ya kushughulikia sakata hilo.

Kesi hiyo itaweka bayana malalamiko juu ya tabia zilizoonyeshwa na wachezaji wao, wakati Serbia pia watahojiwa juu ya kauli za ubaguzi wa rangi zilizotolewa na mashabiki.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.