Watano waangamia katika shambulio la kujitoa mhanga Kabul
Watu wasiopungua watano wameuawa katika shambulio la kujitoa mhanga magharibi mwa mji wa Kabul, shambulio lililotokea leo Jumanne asubuhi, vmamlaka imesema. Huu ni mlipuko wa kwanza baada ya miezi miwili ya utulivu katika mji mkuu wa Afghanistan.
Imechapishwa:
"Mapema subuhi, mshambuliaji wakujitoa mhanga, alijilipua na kuua watu watano wakiwemo raia wawili na askari watatu," Waziri wa Mambo ya Ndani Nasrat Rahimi ameliambia shirika la Habari la AFP.
Shambulio hilo pia limewajeruhi watu kumi na wawili, ikiwa ni pamoja na raia watano, amesema Rahimi, na kuongeza kuwa idadi hii inaweza kubadilika.
Wizara ya Ulinzi imesema katika taarifa kwamba watu watano wameuawa - raia mmoja na wanne kutoka vikosi vya usalama - na sita wamejeruhiwa.
Hakuna kundi ambalo limedaikuhusika na tukio hilo, ambalo lilitokea kwenye eneo la kwanza la ukaguzi kwenye lango la Chuo Kikuu cha jeshi, kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vilivyoshuhudia tukio hilo na maafisa wa usalama.
Mkuu wa polisi wa Kabul amethibitisha shambulio hilo na kudai kuwa yeye ndio alikuwa amelengwa.