Pata taarifa kuu
IRAQ-USALAMA

Kiongozi wa kiroho wa Kishia aunga mkono madai ya waandamanaji Iraq

Watu zaidi ya 40 wamepoteza maisha nchini Iraq baada ya kuzuka kwa makabiliano kati ya polisi na waandamanaji katika maeneo mbalimbali katika taifa hilo lenye utajiri wa mafuta.

Mandamano mabaya yameripotiwa Alhamisi hii Oktoba 3, 2019 nchini Iraq. Hapa  ni katika mji wa Baghdad.
Mandamano mabaya yameripotiwa Alhamisi hii Oktoba 3, 2019 nchini Iraq. Hapa ni katika mji wa Baghdad. REUTERS/Alaa al-Marjani
Matangazo ya kibiashara

Maandamano haya yameendelea licha ya serikali, kutangaza hali ya kutotembea usiku katika mji mkuu Bangdad.

Waandamanaji wanasema wanataka serikali iboreshe huduma mbalimbali kama ukosefu wa mara kwa mara wa umeme na maji.

Makabiliano hayo yamesabisha waandamanaji wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa, baada ya kushambuliwa na risasi za moto, na wengine kulazimishwa kukimbia wakihofia usalama wao.

Umoja wa Mataifa umelaani polisi kutumia nguvu katika maandamano hayo, huku kiongozi wa kiroho wa Kishia Grand Ayatollah Ali Sistan akiitaka serikali kusikiliza madai ya wanadamanaji.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.