Uturuki yaimarisha ulinzi kaskazini mwa Syria
Uturuki imetuma wanajeshi wake Kaskazini mwa Syria katika operesheni ya kupambana na wapiganaji wa Kikurdi.
Imechapishwa:
Serikali ya Uturuki inasema kuwa, wapiganaji hao ni magaidi na ni hatari kwa usalama wa nchi yake.
Wapiganaji hao wanaofahamika kama YPG, ngome yao kuu ni Afrin karibi sana na Uturuki.
Kumeshuhudia makabiliano makali kati ya wanajeshi wa Uturuki na wapiganaji hao, huku kukiwa na wasiwasi wa kutokea kwa maafa zaidi.
Uamuzi huu wa Uturuki huenda ukazua mgogoro kati yake na Marekani ambao inawaunga mkono wapiganaji hao kwa kile inachosema kuwa inasaidia katika vita dhidi ya Islamic State nchini Syria.
Serikali ya Syria inasema Uturuki haikuwaambia kuhusu, operesheni hiyo licha ya serikali ya Ankara kusema kuwa ikuwa imeiambai serikali ya Damascus.