Pata taarifa kuu
IRAQ-ISIS

Iraq yatangaza mapumziko kusherekea ushindi dhidi ya IS

Waziri Mkuu wa Iraq Haider al-Abadi jana Jumamosi ametangaza ushindi dhidi ya kundi la Islamic State nchini humo na kusema kuwa, sasa wanajeshi wa Iraq wanadhibiti kikamilifu mpaka wa nchi hiyo na Syria.

Waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abadi
Waziri mkuu wa Iraq Haider al-Abadi Reuters
Matangazo ya kibiashara

Tangazo hili linakuja baada ya serikali ya Syria kusema kuwa imemaliza kazi ya kupambana na Islamic State nchini Syria.

Mamlaka nchini humo zimetangaza mapumziko ya umma  leo Jumapili kusherehekea ushindi huo huku waziri mkuu Abad katika hotuba yake akiwa wizara ya ulinzi amesema kuwa vita ya sasa nchini humo itakuwa kupambana na rushwa .

Kundi la Islamic State limekuwa likipambana na vikosi vya serikali ya Syria na Iraq tangu mwaka 2014 na lilifanikiwa kudhoibiti maeneo mengi na makubwa nchini humo.

Wakati mamlaka zikitangaza mapumziko ya umma leo Jumapili "kusherehekea ushindi", Abadi alisema katika hotuba ya wizara ya utetezi kuwa vita vya Iraq ijayo itakuwa kushinda janga la rushwa.

Naye kiomngozi wa kiroho wa taifa hilo Ayatollah Ali Khamenei ,ametoa wito wa kuungana pamoja hatua itakayosababisha kuundwa kwa vitengo vya silaha vya Hashed al-Shaabi.

 

 

 

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.