Pata taarifa kuu
SYRIA-IS-USALAMA

Majeshi ya Syria yadhibiti mji wa Al-Bukamal kutoka mikononi mwa IS

Majeshi ya Syria yakisaidiwa na kundi la Hezbollah kutoka Lebanon na wanamgambo wa Iraq wameurejesha tangu siku ya Jumatano jioni mji wa Al-Bukamal kwenye himaya ya serikali kutoka mikononi mwa kundi la Islamic State.

Askari wa jeshi la Syria (Hapa ilikua Deir Ezzor Oktoba 31, 2017).
Askari wa jeshi la Syria (Hapa ilikua Deir Ezzor Oktoba 31, 2017). STRINGER / AFP
Matangazo ya kibiashara

Al-Bukamal ni mji wa mwisho ambao ulikua ukishikiliwa na kundi la Islamic State mashariki mwa Syria. Taarifa ya kuurejesha mji huu kwenye himaya ya serikali imethibitishwa na vyanzo vya serikali vya Syria na shirika la la habari la Urusi la Sputnik.

Jeshi la Syria lilitarajia vita vikali na vya muda mrefu kwa minajili ya kuurejesha kwenye himaya yake mji wa Al-Bukamal, ambapo walikua walijificha wapiganaji wa mwisho wa kundi la Islamic State, ambao walikimbia mkoa wa Syria wa Deir Ezzor na mji wa Iraq wa Al-Qaim. Lakini wapiganaji hao wamepoteza mji huo kwa haraka kuliko ilivyotarajiwa.

Kwa mujibu wa vyanzo vya kijeshi kutoka Syria, Urusi na Syria walitumia uwezo mkubwa katika vita vya kuurejesha mji huo kwenye himaya ya serikali. Kikosi cha wanamaji na kile cha wanaanga walirusha makombora mengi na mabomu wiki mbili zilizopita dhidi ya ngome za kundi la Islamic Islamic.

Pamoja na kupoteza mji wa Al-Bukamal, kundi la Islamic State halina tena mji wowote linaloshikilia nchini Iraq na Syria. Lakini wapiganaji wa kundi hilo wapo katika maeneo makubwa ya jangwani kati ya nchi hizo mbili, ambako wamehifadhi chakula, silaha, na risasi, kwa kutarajia vita ya vya kuvizia katika nchi hizo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.