Pata taarifa kuu
SUDANI KUSINI-WFP-NJAA

WFP: Zaidi ya watu milioni sita wanakabiliwa nanjaa Sudani Kusini

Shirika la Umoja wa mataifa la mpango wa Chakula Duniani,WFP, limetangaza kuwa zaidi ya watu milioni sita wa Sudan Kusini, wanakabiliwa na njaa.

Wakimbizi wa ndani kutoka Sudan kusini wa kambi ya Bentiu wakipokea chakulakilichotolewa na Umoja wa Mataifa.Kusini mwa nchi, wakaazi wanakabiliwa na njaa, Juni 18, 2017.
Wakimbizi wa ndani kutoka Sudan kusini wa kambi ya Bentiu wakipokea chakulakilichotolewa na Umoja wa Mataifa.Kusini mwa nchi, wakaazi wanakabiliwa na njaa, Juni 18, 2017. REUTERS/David Lewis
Matangazo ya kibiashara

Shirika hilo linasema waliokumbwa na njaa ni pamoja na watu wasio na makao na wananchi wa kawaida wanaoishi kwenye vijiji kote nchini Suda

Kwa upande mwengine Shirika la chakula duniani FAO linasema kuwa licha ya hatua ambazo zimeendelea kuchukuliwa na bara la Afrika kukabiliana na hali ya ukame, bado tatizo ni kubwa na linatishia ustawi wa maelfu ya raia.

Wajumbe wa mkutano wa FAO unaoendelea mjini Roma, Italia, wanakubaliana kuwa kasi zaidi inahitajika ili kukabiliana na tatizo la njaa na utapia mlo kwenye nchi za Afrika ikiwa zinataka kufikia malengo endelevu ya mwaka 2025 ya kuwa bara hilo limetokomeza njaa.

Wataalamu wanasema changamoto kubwa imekuwa ni mabadiliko ya tabia nchi ambayo yameendela kusababisha madhara makubwa kwa bara hilo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.