Askari 1,000 wa Burundi kuondoka Somalia Februari 2019
Umoja wa Afrika umesema, wanajeshi 1,000 kutoka Burundi, wataondolewa katika kikosi chake cha AMISOM nchini Somalia kufikia mwisho wa mwezi Februari mwaka 2019.
Imechapishwa:
AU inasema, hatua ni kuhakikisha kuwa nchi zinazochangia wanajeshi nchini Somalia, zinakuwa na wanajeshi sawa.
Uamuzi huu unakuja wakati huu Burundi ikiendelea kuwa na uhusiano mbaya na Umoja wa Afrika kwa sababu ya mzozo wa kisiasa unaoendelea nchini humo.
AMISOM inaundwa na wanajeshi kutoka mataifa matano yaukanda wa Afrika Mashariki na Kati ambayo ni Uganda, Burundi, Ethiopia, Kenya na Djibouti.
Lengo likiwa ni kusaidia kurejesha amani nchini Somalia na kukabiliana na kundi la kigaidi la Al Shabab.