Pata taarifa kuu
SUDAN KUSINI-MACHAR-KIIR

UN na AU zataka mkataba wa amani Sudan Kusini kuanza kutekelezwa haraka

Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika, unazitaka pande zote nchini Sudan Kusini, kuchukua hatua za makusudi kuanza kutekeleza mkataba wa amani uliotiwa saini hivi karibuni.

Salva Kiir na  Riek Machar walipotia saini mkataba tarehe 12 mwezi Septemba 2018
Salva Kiir na Riek Machar walipotia saini mkataba tarehe 12 mwezi Septemba 2018 YONAS TADESSE / AFP
Matangazo ya kibiashara

Jean Pierre Lacroix, kutoka katika jeshi la kulinda amani la Umoja wa Mataifa amezuru nchini humo na kusema utekelezwaji wa mkataba huo utasaidia kuimarisha usalama nchini humo.

Rais Salva Kiir na kiongozi wa waasi, walikubaliana kuunda serikali pamoja na kuunda jeshi moja ili kurejesha amani nchini humo. Hata hivyo, utekelezwaji unafanyika taratibu.

Aidha, ilikubaliwa kuwa Machar atarejea tena katika nafasi yake ya zamani ya kuwa Makamu wa kwanza wa rais.

Dunia inasubiri iwapo mkataba huo utatekelezwa kikamilifu kwa sababu, rais Kiir na Machar wameshindwa kutekeleza mikataba ya amani iliyopita.

Riek na Machar wamekuwa wakilaumiana kuhusu anayevunja mkataba huo wa amani na kunzisha vita mara kwa mara.

Maelfu ya watu wamepoteza maisha katika mzozo wa Sudan Kusini na wengine kuyakimbia makwao.

 

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.