Pata taarifa kuu
SUDAN KUSINI-UNSC-USALAMA

UNSC yatangaza vikwazo dhidi ya waziri wa ulinzi wa Sudan Kusini

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limemwekea vikwazo Waziri wa Ulinzi wa Sudan Kusini Kuol Manyang Juk. Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Afrika Mashariki IGAD imetangaza kuwa inaunga mkono hatua hiyo.

Waziri wa Ulinzi wa Sudan Kusini amechukulia vikwazo na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likimshtumu kuendelea kuchochea vita nchini humo.
Waziri wa Ulinzi wa Sudan Kusini amechukulia vikwazo na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likimshtumu kuendelea kuchochea vita nchini humo. ALBERT GONZALEZ FARRAN / AFP
Matangazo ya kibiashara

Hatua hii imechukuliwa kwa kile kinachoelezwa kuwa Bwana Juk amendelea kusababisha mapigano kuendelea nchini humo.

Baraza hilo linasema, mwaka 2017, Waziri huyo aliwapa silaha wapiganaji wa SPLM-N kushambulia makao makuu ya wapiganaji wa upinzani katika eneo la Pagak.

Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Afrika Mashariki IGAD hivi karibuni ilitangaza kuwa inaunga mkono hatua ya kuwekewa vikwazo viongozi na shakhsia wote wanaokwamisha jitihada za kupatiwa ufumbuzi mgogoro nchini Sudan Kusini.

Sudan Kusini, ambayo ilijitenga na Sudan mwaka 2011, ilitumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2013, baada ya Rais Salva Kiir kumtuhumu makamu wake wa zamani, Riek Machar kwamba alihusika na jaribio la kupindua serikali yake.

Umoja wa Mataifa umeendelea kuonya kuwa yeyote, anayeendelea kusababisha mapigano nchini Sudan Kusini, atawekewa vikwazo.

Machafuko nchini Sudan Kusini yamesababisha vifo maelfu ya watu na wengine mamilioni kuyahama makazi yao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.