Pata taarifa kuu
SUDAN KUSINI-USALAMA

Sudan Kusini: Paul Malong ni muasi wa taifa

Serikali ya Sudan Kusini imemtangaza aliyewahi kuwa mkuu majeshi Jenerali Paul Malong kama muasi wakimtuhumu kuhusika katika mashambulizi mfululizo ya juma lililopita.

Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir.
Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir. REUTERS/Stringer
Matangazo ya kibiashara

Jenerali Malong ambaye aliongoza kampeni ya rais Salva Kiir dhidi ya waasi, kwa muda mrefu alikuwa chini ya ulinzi nyumbani kwake tangu mwezi Mei baada ya rais Kiir kumfuta kazi kutokana na kujiuzulu kwa maofisa kadhaa wa jeshi wakidai kunyanyaswa na ubaguzi wa kikabila.

Hata hivyo mwezi Novemba mwaka jana rais Kiir aliruhusu jenerali Malong kutoka nyumbani kwake na kwenda kuishi uhamishoni nchini Kenya baada ya majadiliano na viongozi wa juu wa kabila la Dinka.

Msemaji wa rais Kiir, Ateny Wek Ateny anamtuhumu jenerali malong kwa kuagiza vikosi vyake kushambulia wanajeshi wa Serikali katika kile anachosema ni kutokana na ushahidi wa sauti waliounasa.

Mke wa Malong, Lucy Ayak amekashifu tangazo hili la Serikali akisema ni uongo uliotengenezwa ili kumtafutia sababu za kumshtaki mume wake.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.