Pata taarifa kuu
KENYA-MADAGASCAR

Polisi nchini Kenya yamkamata mshukiwa wa biashara za dawa za kulevya

Polisi nchini Kenya imemkamata Ndechumia Bilali Kimali mshukiwa wa biashara haramu ya dawa za kulevya baada ya kuwasili jijini Nairobi akitokea nchini Madagascar.

Ndechumia Bilali Kimali mshukiwa wa dawa za kulevya (Aliyevalia fulama ya samawati) baada ya kukamatwa na polisi jijini Nairobi Aprili 10 2017
Ndechumia Bilali Kimali mshukiwa wa dawa za kulevya (Aliyevalia fulama ya samawati) baada ya kukamatwa na polisi jijini Nairobi Aprili 10 2017 Daily Nation
Matangazo ya kibiashara

Kimali anashukiwa kuhusika na Kilomita 7.6 ya Heroin iliyoharibiwa na jeshi la Kenya katika Bahari ya Hindi mwaka 2014.

Mshukiwa huyo alikimbilia nchini Madagascar mwaka 2015 baada ya kuharibiwa kwa dawa hizo.

Joseph Mugwanja, Mkuu wa kitengo cha inteljensia katika uwanja wa ndege amesema mshukiwa huyo anaaminiwa kuingiza na kusafirisha dawa za kulevya ndani ya nje ya nchi hiyo.

Tayari watu wengine watano wamefunguliwa mashitaka mjini Mombasa kwa madai ya kushirikiana na Kimali anayeshukiwa kununua dawa hizo na kutaka kuisafirisha nchini Swaziland wakati ilipokamatwa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.