Pata taarifa kuu
KENYA-UHURU KENYATTA

Rais Uhuru Kenyatta kuhutubia maelfu ya wafuasi wa chama kipya cha Jubilee hii leo

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuhutubia maelfu ya wajumbe wa chama kipya cha Jubilee kilichozinduliwa rasmi hapo jana jijini Nairobi. 

Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiwa na naibu wake William Ruto baada ya kutangaza kuundwa kwa chama kipya cha Jubilee
Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta akiwa na naibu wake William Ruto baada ya kutangaza kuundwa kwa chama kipya cha Jubilee Kenya State House
Matangazo ya kibiashara

Vyama zaidi ya 10 vilivyokuwa vinaunda muungano wa siasa wa Jubilee unaongoza nchini humo vilivunjwa siku ya Alhamisi na kwa mara ya kwanza wajumbe wake wamekutana jana na Naibu wa rais William Ruto.

Akiwahutubia wafuasi wa Jubilee hapo jana naibu rais William Ruto amesema kuwa tukio la kuunganisha vyama hivyo na kuwa chama kimoja inalenga kuwaleta wakenya pamoja na kuwa na chama kitakacho kuwa na ajenda ya kitaifa.

Aidha Ruto amesisitiza kuwa nia ya chama cha Jubilee ni kubadilisha siasa za chuki, utengano, ugomvi na mgawanyiko wa jamii katika nchi ya Kenya.

Chama hiki kipya cha Jubilee kinatarajiwa kutumiwa na rais Uhuru Kenyatta na naibu wake kutetea nyadhifa zao wakati wa uchaguzi Mkuu mwaka ujao.
 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.