Pata taarifa kuu
UN-FAO-CHAKULA-NJAA-AFRIKA

Fahamu namna ya kuisadia dunia kuwa na chakula cha kutosha kufikia 2030

Umoja wa Mataifa unalenga kuwa, kufikia mwaka 2030, uwe umemaliza baa la njaa duniani.

Chakula maarufu sana Afrika Mashariki na Kati, Ugali, nyama na mboga za majani
Chakula maarufu sana Afrika Mashariki na Kati, Ugali, nyama na mboga za majani www.trainingarunner.com
Matangazo ya kibiashara

Kila tarehe 16, Umoja huo hutumia siku hiyo kuhimiza umuhimu wa dunia isiyo na njaa na kuangalia mbinu za kufikia malengo hayo.

Unaweza kufanya nini ili kuwa na dunia isiyikuwa na njaa ?

Epuka matumizi mabaya ya chakula

Iwapo kuna chakula kimebaki, kihifadhi kwa matumizi ya baadaye, usikimwage. Unapokula Mkahawani au hotelini, agiza chakula unachoweza kukimaliza na kikibaki, kibebe uende nacho nyumbani.

Zalisha chakula zaidi

Idadi ya watu duniani inapotarajiwa kukua na kufikia Bilioni 9 kufikia mwaka 2050, wakulima wanastahili kutafuta mbinu  za kisasa  kuzalisha chakula zaidi. Mbinu hizo zitawasadia Wakulima kuzalisha chakula zaidi na kuwasaidia kupata faida.

Kula mlo kamili

Pata mbinu za kupika na kupata mlo kamili, utakaokufanya kuwa na afya njema. Unaweza kupika chakula kama hiki kwa kutumia viungo rahisi. Aidha, unaweza kuwasiliana na Mkulima kuona namna anavyopika chakula chake nyumbani kwake.

Harakati za kampeni

Kila mmoja ana jukumu la kutoa elimu kuhakikisha kuwa, dunia inafahamu umuhimu wa kuwepo kwa chakula na madhara ya njaa. Kufanikiwa katika hili ni muhimu viongozi wa eneo unalohisi na wale wa kitaifa kuhusishwa kikamilifu.

 

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.