UKRAINE-SIASA
Waziri Mkuu wa Ukraine Oleksiy Honcharuk ajiuzulu
Waziri Mkuu wa Ukraine Oleksiy Honcharuk amekabidhi leo Ijumaa barua ya kujiuzulu wa rais Volodimir Zelenski lakini ana mashaka juu ya ukweli wa kujiuzulu kwake.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Uamuzi wake unafuatia mkanda wa sauti yake iliyorekodiwa akimkosowa rais mpya wa nchi hiyo.
Oleksiy Honcharuk amesema hatua yake ya kujiuzulu imenuwia kuondoa shaka juu ya heshima na utiifu alionao kwa rais.
Honcharuk anadaiwa kumuelezea Zelensky kama mtu mwenye ufahamu wa kale kuhusu masuala ya kiuchumi na uwezo mdogo wa kujifunza kuhusu nyanja hiyo.