Kim Jong-un: Niko tayari Marekani kufungua ofisi yake Korea Kaskazini
Akizungumza baada ya kikao cha pili cha ana kwa ana na rais wa Marekani Donald Trump, Kim Jong-un amesema amekwenda nchini Vietnam baada ya yeye kuwa tayari kuendelea na mchakato wa kuachana na silaha za nyuklia katika rasi ya Korea.
Imechapishwa: Imehaririwa:
Ikiwa hakuna uwezekano kwamba Trump na Kim watakubaliana juu mpango wa kuachana na silaha za nyuklia Korea Kaskazini, mkutano wao wa pili baada ya miezi nane unaweza angalau kuwawezesha kutangaza kusitisha rasmi vita kati ya Korea mbili.
Vita kati ya Korea Kaskazini na Korea Kusini (1950-1953) ilimalizika, bila mkataba wa amani.
Wakati wa mazungumzo yao kwa siku ya pili, leo Alhamisi asubuhi, Donald Trump amekumusha kuwa "hakuwa na haraka" kuona Korea Kaskazini ikiachana na mpango wake wa nyuklia.