Pata taarifa kuu
ARMENIA-FRANCOPHONIE-USHIRIKIANO

Mkutano wa Francophonie waanza Armenia

Viongozi wa Mataifa 84 ya jumuiya ya nchi zinazozungumza lugha ya Kifaransa, Francophonie wanakutana nchini Armenia kujadili mambo mbalimbali lakini pia watamchagua katibu mkuu wa taasisi hiyo.

Mkutano wa 17 wa Francophonie unafanyika kuanzia Alhamisi hadi Ijumaa wiki hii Yerevan, mji mkuu wa Armenia.
Mkutano wa 17 wa Francophonie unafanyika kuanzia Alhamisi hadi Ijumaa wiki hii Yerevan, mji mkuu wa Armenia. ©KAREN MINASYAN/AFP
Matangazo ya kibiashara

Waziri wa sasa wa Mambo ya Nje wa Rwanda Louise Mushikiwabo anayeungwa mkono na Ufaransa anapewa nafasi ya kushinda nafasi hiyo licha ya mkanganyiko kuhusu hatua hiyo ya Ufaransa.

Licha ya Rwanda kulaumiwa kuhusu swala la uhuru wa kujieleza baadhi ya serikali za Francophonie zinaunga mkono mgombea wake huku Canada na Quebec ambazo awali zilionekana kumunga mkono Michael Jean zimetangaza kutomuunga mkono mgombea huyo raia wa Canada

Kawaida nafasi hiyo viongozi wa nchi wanachama huteuwa baada ya wagombea kuachiana nafasi, lakini Michael Jean amekataa kuachia nafasi na kutaka mchuano.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.