Pata taarifa kuu
KOREA KASKAZINI-USALAMA

Korea Kaskazini yaanza kuharibu silaha zake za nyuklia

Katika rasi ya Korea, maandalizi yanaendelea kwa ajili ya kuharibu kituo kikuu cha majaribio ya silaha za nyuklia cha Korea Kaskazini. Serikali ya Kim Jong-un imealika vyombo vya habari kumi vya kigeni kuhudhuria moja kwa moja zoezi hilo la kuharibu vituo vilivyotumika katika milipuko sita ya nyuklia ya ardhini tangu mwaka 2006.

Waandishi wa habari wa Korea Kusini wakiwasili katika uwanja wa ndege wa Wonsan wakitokea Seoul, Mei 23, 2018.
Waandishi wa habari wa Korea Kusini wakiwasili katika uwanja wa ndege wa Wonsan wakitokea Seoul, Mei 23, 2018. News1 via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Serikali ya Korea Kaskazini imealika waandishi wa habari kutoka nchi mbalimbali thelathini tano: Marekani, China, Urusi, Korea Kusini na Uingereza.

Wamekuja kuhudhuria milipuko hiyo ya kuharibu vituo hivyo vya majaribio, Kaskazini-Mashariki mwa nchi, kwenye kituo hicho kikuu, kwenye mlima, ambapo serikali ilitekeleza milipuko sita ya kinyuklia tangu mwaka 2006 hadi mwaka jana.

Lakini waandishi hawa wa habari wa kigeni wako chini ya uangalizi mkali na hawana uwezo wowote wa kuendesha kazi halisi ya uchunguzi.

Baada ya kuwasili kwao katika Uwanja wa Ndege wa Wonsan, simu zao na vifaa vyao mbalimbali vimechukuliwa na mamlaka husika, amesema mwandishi kutoka kituo cha Sky News kutoka Uingereza.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.