Marekani na washirika wake wakubaliana kuchukua hatua dhidi ya Korea Kaskazini
Marekani na washirika wake wanasema kwa pamoja watachukua hatua kuzuia Korea Kaskazini kuendelea kutengeza silaha za nyuklia lakini pia kuzuia usafirashaji haramu baharini.
Imechapishwa:
Waziri wa Mambo wa nje wa Marekani Rex Tillerson na wenzake wa Canada Chrystia Freeland wamekutana jijini Vancouver na kuwaomba viongozi wengine wa dunia kuunga mkono juhudi zao.
Mkutano huo pia umewakutanisha Mawaziri kutoka Korea Kusini na Japan na kwa mara nyingine kuja na msimamo mmoja wa kuzuia Korea Kaskazini kuendelea na mradi wake wa nyuklia.
Mataifa hayo yamekubaliana kuzuia kwa pamoja usafirishwaji wa vifaa vinavyosaidia Korea Kaskazini kuendelea na mradi wake wa nyuklia wanaosema ni hatari kwa usalama wa dunia.
China na Urusi hawakualikwa katika mkutano huo kutokana na msimamo wao wa kuiunga mkono Korea Kaskazini.