Rais wa zamani wa Georgia aokolewa na wafuasi wake
Rais wa zamani wa Georgia Mikheil Saakashvili ameokolewa na umati wa watu kutoka mikononi mwa polisi, baada ya kukamatwa katika mji mkuu Kiev akishtumiwa kusaidia kundi la kigaidi.
Imechapishwa:
Bw. Saakashvile anakabiliwa na kifungo cha hadi miaka mitano jela ikiwa atapatikana na hatia.
Polisi haijaugumza lolote kufuatia kukombolewa kwa Bw Saakashvili.
Akiwa na pingu kwenye mkono mmoja na akizungukwa na mamia ya watu, Bw Saakash
Bw Saakashvili mwenye umri wa miaka 49, aliutaka umati kumuandoa madarakani rais Petro Poroshenko ambaye ni mshirika wake wa zamani.
Anamlaumu rais Poroshenko kwa kushindwa kumaliza ufisadi. Bw Porokoshenko amekana madai. Saakashvili amekuwa mkosoaji mkubwa wa rais Poroshenko.
Alipewa uraia wa Ukrain mwaka 2015 hatua iliyosababisha apoteze uraia wake wa Georgia.