Mikheil Saakashvili: Napaswa kuhaki yangu kama raia wa Ukraine
Rais wa zamani wa Georgia Mikheil Saakashvili akiwa na wafuasi wake wameingia nchini Ukraine kwa nguvu, licha ya nchi hiyo kumpkonya uraia.
Imechapishwa:
w. Saakashvili amesema ameamua kurudi nchini Ukraine ili kwenda Mahakamani, kupinga kupokonywa uraia wake kwa sababu anataka kurejea katika ulingo wa kisiasa nchini humo.
Bw. Saakashvili ambaye awali alikuwa ni raia wa Georgia na kisha raia wa Ukrain kwa sasa hana uraia wa nchi yoyote baada ya uraia wake wa Ukrain kufutwa na mshirika wake wa zamani raid Petro Poroshenko.
Mikheil Saakashvili alisema kuwa alisukumwa bila kutarajia kwenye mpaka na umati wa watu waliokuwa wamekasirika kutokana na kufungwa kwa mpaka.
Maafisa nchini Ukraine wanasema kuwa aliiangia nchini humo kinyume na sheria na walinzi 15 na mpaka walijeruhiwa.
Wachambuzi wa siasa nchini Ukraine wanasema kuwa rais huyo wa zamani wa Georgia aliyeongoza kati ya mwaka 2004 hadi 2013 anaonekana kuwa mpinzani mkubwa wa rais Petro Poroshenko.