Naibu Mwanasheria mkuu wa Marekani Rod Rosenstein ajiuzulu
Naibu Mwanasheria mkuu wa Marekani, Rod Rosenstein ambaye alisimamia uchunguzi maalumu uliokuwa unafanywa na Robert Mueller ikiwa Urusi iliingilia uchaguzi wa mwaka 2016, ametangaza kujiuzulu nafasi yake.
Imechapishwa:
Rosenstein ambaye tangu rais Donald Trump aingie madarakani hawajawa na uhusiano mzuri, ataondoka kwenye nafasi yake ifikapo Mei 11, uamuzi ambao ulikuwa umetarajiwa kwa muda mrefu.
Kwenye barua yake, Rosenstein amempongeza rais Trump na hata kusifu namna amekuwa mtu wa utani wakati walipokuwa wakikutana.
Rosenstein ambaye alichaguliwa wakati wa utawala wa rais George Bush, alikuwa akitarajiwa kujiuzulu tangu mwezi Machi baada ya William Barr kuteuliwa kama mwanasheria mkuu.
Katika utawala wake ni mara moja tu rais Trump aliwahi kuchapisha picha ya Rosenstein akiwa kwenye mfano wa jela kwa makosa ya uhaini.