Pata taarifa kuu
MAREKANI-HAKI

Naibu Mwanasheria mkuu wa Marekani Rod Rosenstein ajiuzulu

Naibu Mwanasheria mkuu wa Marekani, Rod Rosenstein ambaye alisimamia uchunguzi maalumu uliokuwa unafanywa na Robert Mueller ikiwa Urusi iliingilia uchaguzi wa mwaka 2016, ametangaza kujiuzulu nafasi yake.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Marekani Rod Rosenstein katika mkutano na waandishi wa habari akitangaza kuwafungulia mashtaka maafisa12 wa Urusi Kirusi 12 huko Washington tarehe 13 Julai 2018.
Naibu Mwanasheria Mkuu wa Marekani Rod Rosenstein katika mkutano na waandishi wa habari akitangaza kuwafungulia mashtaka maafisa12 wa Urusi Kirusi 12 huko Washington tarehe 13 Julai 2018. REUTERS/Leah Millis
Matangazo ya kibiashara

Rosenstein ambaye tangu rais Donald Trump aingie madarakani hawajawa na uhusiano mzuri, ataondoka kwenye nafasi yake ifikapo Mei 11, uamuzi ambao ulikuwa umetarajiwa kwa muda mrefu.

Kwenye barua yake, Rosenstein amempongeza rais Trump na hata kusifu namna amekuwa mtu wa utani wakati walipokuwa wakikutana.

Rosenstein ambaye alichaguliwa wakati wa utawala wa rais George Bush, alikuwa akitarajiwa kujiuzulu tangu mwezi Machi baada ya William Barr kuteuliwa kama mwanasheria mkuu.

Katika utawala wake ni mara moja tu rais Trump aliwahi kuchapisha picha ya Rosenstein akiwa kwenye mfano wa jela kwa makosa ya uhaini.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.