Pata taarifa kuu
VENEZUELA-SIASA-UCHUMI

Maduro atangaza mgawo wa umeme kwa siku 30

Rais wa Venezuela Nicolas Maduro, ametangaza siku 30 za mgawo wa umeme. Venezuela imeenelea kukabiliwa na uhaba wa umeme kufuatia kutwa kwa Nishati hiyo ya umeme.

Kiza kinene chaendelea kuukumba mji mkuu wa Venezuela,  Caracas, na miji mingine ya nchi hiyo.
Kiza kinene chaendelea kuukumba mji mkuu wa Venezuela, Caracas, na miji mingine ya nchi hiyo. REUTERS/Carlos Garcia Rawlins
Matangazo ya kibiashara

Aidha, amesema muda wa kufanya kazi unapunguzwa na shule zitaendelea kufungwa kwa sababu ya ukosefu wa nguvu za umeme katika taifa hilo.

Hata hivyo, ameahidi kuwa serikali yake itahakisha kuwa wananchi wanapata huduma ya maji.

Serikali ya Maduro imeendelea kukumbwa na mzozo wa kiuchumi na kisiasa, huku Marekani ikimwekea rais Maduro vikwazo na kutomtambua kama kiongozi wa nchi hiyo.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.