Pata taarifa kuu
KOREA KASKAZINI-KOREA KUSINI-MAREKANI

Korea Kaskazini yataka mazungumzo na Marekani kuendelea

Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un, anataka mkutano wake na rais wa Marekani Donald Trump kuendelea mwezi ujao nchini Singapore kama ilivyopangwa.

Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in akikumbatiana na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un walipokutana katika eneo la mpaka la  Panmunjom, 26 Mei 2018
Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in akikumbatiana na Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un walipokutana katika eneo la mpaka la Panmunjom, 26 Mei 2018 The Presidential Blue House /Handout via REUTERS
Matangazo ya kibiashara

Kim Jong Un, amekutana na rais wa Korea Kusini Moon Jae-in, ambaye amesema uongozi wa Korea Kaskazini bado una nia ya kutokuwa na maeneo ya kutengeza silaha za nyuklia.

Kauli hii ya kiongozi huyo wa Kaskazini, imekuja wakati huu rais Trump akisema bado wanaendelea kuzungumza na maafisa wa Pyongyang na huenda mazungumzo hayo yakaendelea kama ilivyopagwa.

Wiki hii, rais Trump alijiondoa kwenye mazungumzo hayo, baada ya kusema kuwa, matamshi yenye ukali na yaliyoonekana kuwa ya  chuki, kutoka Korea Kaskazini yasingemwezesha kuja katika meza ya mazungumzo.

Hata hivyo, matamshi ya rais Trump siku ya Jumamosi kwamba mambo yanakwenda vizuri, huenda viongozi hao wakakutana tarehe 12 mwezi Juni kama ambavyo ilikuwa imepangwa.

Korea Kaskazini pamona na kutaka mkutano huo, imeonekana kutokubaliana na msimamo wa Marekani kuwa iachane  kabisa na mradi wake wa nyuklia, suala ambalo linaendelea kuwa tata.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.