Pata taarifa kuu
COLOMBIA-FARC-HAKI

Mkuu wa zamani wa waasi wa FARC akamatwa Colombia

Mkuu wa zamani wa waasi wa FARC na mjumbe wa vyama vya amani nchini Colombia yuko mikononi mwa polisi mjini Bogota tangu jana Jumatatu. Kwa mujibu wa mwendesha mashitaka, Seúxis Hernández, mwenye umri wa miaka 50, Jesús Santrich, aliongoza biashara ya madawa ya kulevya baada ya kusaini mkataba.

Jesús Santrich, mmoja wa viongozi wa zamani wa FARC hapa ilikua mnamo mwezi Novemba 2017, alikamatwa Jumatatu, Aprili 9, 2018 huko Bogota na polisi kwa kosa la kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya.
Jesús Santrich, mmoja wa viongozi wa zamani wa FARC hapa ilikua mnamo mwezi Novemba 2017, alikamatwa Jumatatu, Aprili 9, 2018 huko Bogota na polisi kwa kosa la kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya. REUTERS/Jaime Saldarriaga
Matangazo ya kibiashara

Kulingana na mashtaka hayo, ushahidi ulitolewa na Marekani, ambayo inataka asafirishwe hadi katika jel aya zamani. FARC, chama cha siasa kupitia makubaliano ya amani, kimekataa kusirikiana na rais wa zamani Uribe, aliyepinga mkataba wa amani.

"Sintosumbuka kwa sababu Jesús Santrich kakamatwa," Rais Juan Manuel Santos alisema kwenye televisheni siku ya Jumatatu. Mwendesha mashitaka wa Colombia ana "ushahidi wa kutosha" dhidi ya machafuko ya zamani ambapo alihusika Santrich katika biashara ya madawa ya kulevya baada ya kusaini makubaliano ya amani mnamo mwezi Novemba 2016, kwa mujibu wa rais wa Colombia.

Sheria imefanya kazi yake, amesema Juan Manuel Santos , akibaini "tulizunguzma amani na wahalifu, kama vile Ivan Duque, mbwa wa rais wa zamani Uribe, na mgombea wa urais katika uchaguzi wa Mei 27.

Jesús Santrich, ambaye alikuwa amejizolea sifa nyingi katika mazungumzo ya amani, aliteuliwa mwezi Agosti kuwa seneta, chini ya makubaliano ya amani ambayo yalitoa nafasi 10 bungeni kwa kundi la zamani waasi la FARC.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.