Raia 40 wa Marekani waambukwiza virusi vya Corona katika meli ya “Diamond Princess”
Marekani imewarudisha nyumbani raia wake, waliokuwa wamekwama ndani ya Meli, iliyokuwa na watu walioambukizwa na virusi vya Corona nchini Japan, wakati huu, idadi ya watu waliopoteza maisha, ikiongezeka na kufikia zaidi ya 1,700.
Imechapishwa:
Ripoti zinasema kuwa, ndege mbili zilizowabeba raia wa Marekani, waliokuwa ndani ya meli hiyo iliyokuwa imetengwa, zimeondoka katika uwanja wa Haneda jijini Tokyo nchini Japan.
Wamarekani waliokuwa ndani ya meli hiyo iliyokuwa imezuiwa, walikuwa 400, na wamekuwa katika hali hiyo tangu tarehe 3 mwezi Februari.
Katika hatua nyingine, licha ya maafisa nchini China kusema kiwango cha maambukizi kinapungua, inaripotiwa kuwa idadi ya watu waliombukizwa virusi hivyo kufikia siku ya Jumatatu ni zaidi ya 70,500.
Idadi kubwa ya maambukizi hayo, yanasalia katika mji wa Wuhan katika jimbo la Hubei, wakati huu Shirika la Afya Duniani, WHO, likisema kwa sasa ni vigumu kueleza ni lini maambukizi haya yatafika mwisho.