NEW-ZEALAND-MAJANGA ASILI
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.2 lapiga kaskazini mwa New Zealand
Tetemeko la ardhi lenye la ukubwa wa 6.2 katika vipimo vya Richter limepiga leo Jumanne asubuhi kaskazini mwa kisiwa cha New Zealand, shirika la Marekani linalohusika na masuala ya majanga asili (USGS) limebaini.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kitovu cha tetemeko hilo kimegunduliwa kwenye urefu wa kina wa kilomita 228, karibu kilomita 63 mashariki mwa mji wa New Plymouth upande wa magharibi wa kisiwa.
Hakuna hasara yoyote iliyotokea wala dalili zozote za Tsunami kwa mujibu wa USGS.
Kisiwa cha New Zealand kimekuwa kikikabiliwa na majanga ya asili, na hali hiyo imekuwa ikisababisha uharibifu mkubwa.