Pata taarifa kuu
INDIA-MAJANGA ASILI

Mvua zaua watu zaidi ya 78 nchini India

Mvua kubwa zimeua watu wasiopungua 78 kaskazini na magharibi mwa India, serikali ya nchi hiyo imetangaza. Watu wengi wamepoteza makazi yao kutokana na mvua hizo zinazoendelea nchini humo.

kijiji kidogo cha jimbo la Rajasthan, India ambapo watu zaidi ya 78 wamepoteza maisha kutokana na mvua kubwa zinazonyesha.
kijiji kidogo cha jimbo la Rajasthan, India ambapo watu zaidi ya 78 wamepoteza maisha kutokana na mvua kubwa zinazonyesha. Vincent Desjardins
Matangazo ya kibiashara

Watu thelathini na watatu walipoteza maisha siku ya Jumatano wiki hii katika jimbo la magharibi la Rajasthan na wengine 45 walipoteza maisha katika jimbo la Uttar Pradesh, kaskazini mwa nchi.

"Tumekumbwa na mvua kubwa yenye upepo usio wa kawaida hali ambayo ilisababisha watu 33 kupoteza maisha katika maeneo ya Alwar, Dholpur na Bharatpur, katika jimbo la Rajastan" amesema Hemant Gera, Afisa wa Idara ya huduma za dharura katika jimbo la Rajasthan.

Mvua hizo pia zimeathiri maeneo ya Saharanpur, Bareilly, Bijnore na Agra katika jimbo la Uttar Pradesh.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.