Pata taarifa kuu
SUDAN-ETHIOPIA-MISRI-USHIRIKIANO

Sudan, Ethiopia, Misri, wafikia makubaliano ya matumizi ya Mto Nile

Jitihada zinaendelea kupigwa kati ya Ethiopia, Misri na Sudan katika mazungumzo ya matumizi ya maji ya Mto Nile. Nchi hizo tatau zimekubaliana kutumia maji ya Mto huyo Nile

Ethiopia na Misri zimekuwa zikizozana tangu Ethiopia ilipoanza kujenga bwawa la Grand Renaissance mwaka 2011.
Ethiopia na Misri zimekuwa zikizozana tangu Ethiopia ilipoanza kujenga bwawa la Grand Renaissance mwaka 2011. REUTERS/Tiksa Negeri
Matangazo ya kibiashara

Mazungumzo hayo yanayongozwa na Marekani, na pande zote zilikuwa zimekubaliana kuwa kufika jana mwafaka uwe umepatikana, lakini Mawazier wa Mambo ya nje wa mataifa hayo matatu sasa wasema kufikia tarehe 28 au 29 mwezi huu mkataba utakuwa umefikiwa.

Taarifa ya pamoja iliyotolewa na nchi tatu, pamoja na Marekani na Benki ya Dunia, imesema kwamba washiriki wanaojadiliana wamekubaliana kujaza bwawa la Grand Renaissance linalojengwa Ethiopia wakati wa msimu mvua kati ya miezi ya Julai na Agosti.

Hata hivyo taarifa hiyo haikusema lolote kuhusu masuala ya msingi yanayozunguka mgogoro huo ambayo ni kasi ya kujaza bwawa hilo

Ethiopia inatumia maji ya Mto Nile kujenga bwawa kubwa la kuzalisha umeme, huku Misri ikilalamika kuwa, hatua hiyo itasaiabibisha wananchi wake kukosa maji kwa sababu mto huo ndio chanzo pekee cha maji.

Makubaliano ya mwisho yatatiwa saini Januari 28-29, wakati ambapo mawaziri kutoka nchi tatu watakuwa wanakutana Washington.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.