Pata taarifa kuu
UGIRIKI-LIBYA-UDALAMA-AMANI

Ugiriki yataka kusaidia kuokoa mchakato wa amani Libya

Ugiriki inasema inataka pia kuhusishwa katika mzozo wa Libya, wakati huu Uturuki ikionekana kuchukua usukani wa kulisaidia taifa hilo la Afrika Kaskazini kuwa salama.

Libya yaendelea kukumbwa na mapigano kati ya jeshi la erikali ya Tripoli na vikoi vya Jenerali Khalifa Haftar.
Libya yaendelea kukumbwa na mapigano kati ya jeshi la erikali ya Tripoli na vikoi vya Jenerali Khalifa Haftar. Mahmud TURKIA / AFP
Matangazo ya kibiashara

Kauli ya Ugiriki, imetolewa na serikali ya nchi hiyo ambayo inasema iwapo haitahusika, huenda eneo la Meditterian likaathirika na mzozo huo. Kwa upande mwengine Uturuki inasema inataka kutuma jeshi lake kuisaidia serikali ya Libya inayotambuliwa kimataifa, dhidi ya makundi ya wapinzani.

Hayo yanajiri wakati serikali ya Libya yenye makao yake mjini Tripoli inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imekanusha kuwa inasaidiwa na kikosi cha waasi wa Syria wanaoungwa mkono na Uturuki.

Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki ametahadharisha kwamba mgogoro wa nchini Libya unaweza kutumbukia katika vurumai na kwamba nchi hiyo inaweza kugeuka Syria nyingine. Waziri huyo Mevlut Cavusoglu amesema hayo wakati akifanya juhudi kwa lengo la kupitisha sheria ya kuiwezesha Uturuki kupeleka majeshi nchini Libya.

Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan anakutana na Waziri Mkuu wa Libya anayetambuliwa kimataifa Fayez al-Sarraj huko Istanbul, Uturuki, Novemba 27, 2019.
Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan anakutana na Waziri Mkuu wa Libya anayetambuliwa kimataifa Fayez al-Sarraj huko Istanbul, Uturuki, Novemba 27, 2019. © Presidential Press Office/Handout via REUTERS

Waziri Cavusoglu amesema ikiwa Libya itageuka kuwa Syria nyingine na nchi zote za kanda zitaathirika

Serikali ya Libya inayotambuliwa rasmi na Umoja wa Mataifa imekuwa inakabiliana na majeshi ya jenerali muasi Khalifa Haftar yanayoungwa mkono na Urusi, Misri, Umoja wa Falme za Kiarabu na Jordan.

Majeshi ya Jenerali muasi Haftar mpaka sasa bado hayajaweza kuingia mjini Tripoli lakini taarifa zinasema vikosi vyake vimepata mafanikio ya kiasi fulani kusinimwa mji huo kutokana na msaada wa wapiganaji kutoka Urusi na Sudan.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.