Pata taarifa kuu
KENYA-SOMALIA-USALAMA-SIASA-ALSHABAB

79 wauawa katika shambulizi mjini Mogadishu

Idadi ya vifo vilivyotokana na Mlipuko mkubwa wa bomu lililokuwa limetegwa katika eneo lenye shughuli nyingi mjini Mogadishu nchini Somalia imeongezeka na kufikia 79 na majeruhi kadhaa,likiwa ni shambulizi jingine baya ndani ya miaka miwili nchini humo.

Waokoaji wakiondoa mabaki ya miili ya watu  katika eneo la mkasa
Waokoaji wakiondoa mabaki ya miili ya watu katika eneo la mkasa Reuters
Matangazo ya kibiashara

16 kati ya waliofariki walikuwa wanafunzi kutoka katika chuo kikuu cha Binafsi Banadir kilichopo mjini Mogadishu waliokuwa safarini mara mlipuko ulipotokea kusini magharibi mwa jiji hilo.

Majeruhi wengi walibebwa kwa machela na kuondolewa katika eneo la mkasa ambapo mlipuko ulivuruga na kusalia mabaki ya magari.

Raia 2 wa Uturuki ni miongoni mwa waliouawa,kulingana na wizara ya mambo ya kigeni ya Uturuki ambayo iliarifu kupitia ukurasa wake wa Twita.

Bado haijajulikana nani hasa wahusika wa shambulizi hilo licha ya mashambulizi kadhaa kutekelezwa na kundi la kiislamu Al shabab ambalo limekuwa likipambana na serikali inayoungwa mkono na umoja wa mataifa.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.