Pata taarifa kuu
UGANDA-DRC-SIASA-DIPLOMASIA

Uganda na DRC zakubaliana kushiriki katika masuala ya usalama na biashara

Mataifa jirani ya Uganda na DRC yamekubaliana kushirikiana katika mikataba kadhaa ya maendeleo na usalama.

Rais wa DRC  Félix Tshisekedi  akiwa na mwenzake wa Uganda  Yoweri Museveni, katika Ikulu ya Entebbe Novemba 09 2019
Rais wa DRC Félix Tshisekedi akiwa na mwenzake wa Uganda Yoweri Museveni, katika Ikulu ya Entebbe Novemba 09 2019 Sumy Sadurni / AFP
Matangazo ya kibiashara

Umekuwa ni mkutano wa kwanza wa kibiashara na uwekezaji kati ya nchi hizo mbili, na kuhudhuria rais Felix Tshisekedi akiambatana na ujumbe wa watu 117 wakiwemo Mawaziri.

Miongoni mwa mambo yaliyokubaliwa katika mkutano huo ni kwa Kampala na Kinshasa kushirikiana katika masuala ya miundo mbinu, biashara na uwezekaji pamoja na ulinzi na usalama.

Katika mkutano huo, rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema, anaunga mkono ombi la DRC kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuungana na mataifa mengine kama Kenya, Uganda, Tanzania, Burundi, Rwanda na Sudan Kusini.

Uhusiano wa Uganda na DRC katika miaka iliyopita, ulionekana kuwa mbaya lakini tangu kuingia madarakani kwa rais Tshisekedi mwezi Januari, mambo yameanza kubadilika huku nchi hizo mbili zikiahidi kushirikiana zaidi.

Baada ya ziara yake nchini Uganda, rais Tshisekedi anakwenda jijini Paris kukutana na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.