Pata taarifa kuu
GUINEA BISSAU-ECOWAS-SIASA-USALAMA

ECOWAS: Hatua ya José Mario Vaz ya kuvunja serikali ni kinyume na sheria

Taarifa ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS, iliyotolewa Jumanne wiki hii inabaini kwamba serikali iliyovunjwa Jumatatu na Rais José Mario Vaz ni matokeo ya uamuzi wa mkutano wa kilele wa jumuiya hiyo uliyofanyika Juni 29, 2019.

José Mário Vaz, Rais wa Guinea-Bissau
José Mário Vaz, Rais wa Guinea-Bissau SEYLLOU / AFP
Matangazo ya kibiashara

Mkutano huo, ECOWAS inasema, ulibaini kwamba muhula wa José Mario Vaz ulimalizika mwishoni mwa Juni, na hiyo inaweza kusababisha kukosekana kwa serikali halali na hivyo kusababisha mkwamo katika shughuli za serikali.

Wakati huo huo ECOWAS inaona kwamba hatua ya Rais José Mario Vaz ya kuvunja serikali ni kinyume cha sheria wakati hana mamlaka yoyote ya kuchukuwa hatua yoyote ile.

ECOWAS katika taarifa yake inasema inauunga mkono timu ya waziri mkuu aliyefukuzwa kazi Aristide Gomez na inamtaka waziri huyo mkuu kuendelea na maandalizi ya uchaguzi wa urais uliopangwa kufanyika Novemba 24.

ECOWAS imebaini kwamba ikiwa zimesalia wiki tatu kabla ya uchaguzi, hakuna sababu ya kusimamisha mchakato wa uchaguzi, hali ambayo inaweza kusababisha nchi inatumbukia katika machafuko zaidi.

"Mtu yeyote ambaye kwa njia yoyote atahatarisha mchakato wa uchaguzi, atakabiliwa na vikwazo," ECOWAS imeonya.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.