Maswali mengi yaibuka kuhusu ajali ya ndege ya serikali DRC
Rais wa DRC Felix Tshisekedi Tshilombo amekutana na familia ya waathiriwa wa ajali ya ndege ya serikali Antonov 72. Dereva wake na maafisa wake kadhaa wa ulinzi walikuwa katika ndege hiyo.
Imechapishwa:
Ofisi ya rais ilithibitisha rasmi Jumanne wiki hii kuwa mabaki ya ndege hiyo yamepatikana katika eneo la Sankuru na kuahidi kufanya kilio chini ya uwezo wake ili ukweli kuhusu mazingira ya ajali hiyo ujulikane.
Miili ya kwanza iliyopatikana karibu na mabaki hayo yamesafirishwa na kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini DRC, MONUSCO.
Mamlaka imethibitisha kuwa miili ya watu wanne imepatikana, huku rubani amethibitishwa kupatikana akiwa hai.
Maswali yameibuka kuhusu ajali ya ndege hiyo ya jeshi la DRC, ambayo ilikuwa imetumiwa na ofisi ya rais kwa kusafirisha gari ya rais na walinzi wake wa karibu Mashariki mwa DRC.
#RDC #Antonov: Vitaly Shumkov pourrait avoir été arrêté en Thailande en 2010, accusé de transporter des armes nord-coréennes - https://t.co/NfbuEPYDO3 Vladimir Sadovnichy pourrait avoir été condamné en 2011 au Tadjikistan pr trafic dps l’Afghanistan - https://t.co/0WB0KrGz21 4/4
Sonia Rolley (@soniarolley) October 16, 2019
Ndege hiyo ilipotea siku ya Alhamisi ikiwa na watu watano, mmoja wapo akiwa dereva maalumu wa rais Tshisekedi.
Awali palikua na taarifa kinzani kuhusu mahali ndege hiyo ilipo pamoja na idadi ya watu waliokuwemo.