Pata taarifa kuu
AFRIKA KUSINI-MAREKANI-UCHUMI

Washington yaweka vikwazo dhidi ya familia ya Gupta

Marekani imeweka vikwazo dhidi ya familia tajiri ya Gupta, inayohusishwa kwa kashfa ya ufisadi nchini Afrika Kusini, Wizara ya Fedha ya Marekani imetangaza katika taarifa Alhamisi wiki hii.

Verun Gupta (kushoto) na Ronica Ragovam, wawili wa watuhumiwa wanaohusishwa na uchunguzi wa madai ya ufisadi unaolenga familia ya Gupta, katika mahkama ya Bloemfontein Februari 14.
Verun Gupta (kushoto) na Ronica Ragovam, wawili wa watuhumiwa wanaohusishwa na uchunguzi wa madai ya ufisadi unaolenga familia ya Gupta, katika mahkama ya Bloemfontein Februari 14. CHARL DEVENISH / AFP
Matangazo ya kibiashara

Ajay, Atul na Rajesh Gupta, wanaoshtumiwa kuhusika "katika kashfa kubwa ya ufisadi na hongo ili kupata mikataba ya serikali" wamewekwa kwenye orodha nyeusi ya vikwazo.

Familia ya Gupta, ambayo ilikuwa na uhusiano wa karibu na rais wa zamani wa Afrika Kusini Jacob Zuma, inatuhumiwa "kuiba mamia ya mamilioni ya dola kupitia miradi haramu na serikali," Wizara ya Fedha ya Marekani imeaongeza.

Familia hiyo ya Gupta imekuwa kwenye shutuma za muda mrefu kuhusu kutumia urafiki wao na rais Jacob Zuma kujinufaisha kisiasa kwaajili ya manufaa ya biashara zao.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.