Pata taarifa kuu
SUDANI-UFARANSA-USALAMA-UGAIDI

Ufaransa kusaidia Sudan kuondolewa katika orodha ya nchi zinazofadhili ugaidi

Waziri wa Mambo ya nje wa ufaransa Jean-Yves Le Drian akiwa jijini Khartounm nchini Sudan amesema nchi yake itaendelea kuweka shinikizo ili Sudani iondolewe katika nchi ambazo zimeorodheshwa na Marekani, kuwa zinafadhili ugaidi.

Jenerali Abdel Fattah al-Burhan akila kiapo kama rais wa Baraza Kuu tawala nchini Sudan, Khartoum Agosti 21, 2019.
Jenerali Abdel Fattah al-Burhan akila kiapo kama rais wa Baraza Kuu tawala nchini Sudan, Khartoum Agosti 21, 2019. SUDAN PRESIDENTIAL PALACE / AFP
Matangazo ya kibiashara

Le Drian amekuwa nchini Sudani na kuwa kiongozi wa juu wa Ufaransa kuzuru taifa hilo baada ya miaka 10, na ziara hii imekuja, baada ya mabadiliko ya uongozi nchini Sudani.

Hivi karibuni Waziri Mkuu Abdallah Hamdok alifanikiwa kuunda serikali ambayo inajumuisha raia wa kawaida na jeshi.

Hayo yamekuja baada ya jeshi na viongozi wa maandamano kuafikiana kuhusu suala la kugawana madaraka.

Maelfu ya raia waliuawa katika maandamano ya kumng'atua madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo Omar Hassan Al Bashir ambaye kwa sasa anakabiliwa na mkono wa sheria.

Kusambaza :
Ukurasa haipatikani

Maudhui unayojaribu kuyatafuta hayapatikani kwa sasa au yamekwishaondolewa.