ZIMBABWE-SIASA-USALAMA
Mkosoaji wa Mnangagwa atekwa nyara na baadae kuachiliwa
Mchekeshaji wa mitandaoni nchini Zimbabwe Samantha Kureya, maarufu kwa jina la 'Gonyeti' ametekwa na watu wasiojuliakana akiwa nyumbani kwake jijini Harare.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Ripoti zinasema kuwa baada ya kutekwa alipigwa na kujeruhiwa vibaya.
Kureya ambaye pia ni mwanahabari ameelezea namna wanaume watatu waliokuwa wamefunika nyuso zao walivyovamia nyumba yake na kumchukua kwenda kumtesa.
Amekuwa mkosoaji wa serikali ya Emmerson Mnanangwanga na jeshi la polisi kupitia vichekesho vyake.