SUDANI-SIASA-HAKI
Sudan yaombwa kumuachilia huru mwanahabari Michael Christopher
Mke wa Mwanahabari maarufu nchini Sudan Kusini Michael Christopher, anaomba maafisa wa usalama kumwachilia huru mume wake au kumfungulia mashtaka Mahakamani.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Christopher ambaye ni Mhariri wa Gazeti la Kiarabu la Al Watan, amekuwa akizuiwa na maafisa wa usalama tangu wiki iliyopita.
Alikamatwa wakati akisafiri kwenda jijini Nairobi, nchini Kenya, kupata matibabu na pasi yake ya kusafiria kuchukuliwa.
Marekani na mashirika ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu, pia yanataka aachiliwe huru.